Showing posts with label fid q. Show all posts
Showing posts with label fid q. Show all posts

kemosabe by Fid Q

Niliamini mapene hayatoshi..na niki-hustle siyakosi/
Sababu.. sipo kwenye loss na life simple huwa hai-cost/
Kwahivyo nikaenda Dar na treni… of thoughts../
Sikwenda kuzubaa au kushangaa nikusaka chapaa boss/
Sikutaka kuivaa mikosi..nilitaKa kuivaa mikoti/
Sikuwa na passport..password.. pin..lakini ni crack codes/
Walionisapoti wote siwaoni kwa line/
Wakini-approach ili nifungue pochi ya noti tu-shine..hatuko fine/
Je mimi ni kaka mubaya…? kaka aso haya../
KAKA..? huniitaga NAKAAYA/
Mama C huniita brother bila shaka.. Mozaya/
Niko sick & tired of being sick & tired/
Na huu ni mwaka wa ndui/ Sitaki upele urudi tena.. mnachotaka sikijui/
Nashukuru hamtopata mbawa ikiwa mtaupata huo uchui/
Mnautaka uadui? mnayempaka ni mtata.. makaka hamkui?
Mmeendekeza hila.. legeza hasira za harakati/
Mie nita-ball…. hata kwa mpira wa makaratasi/
Unaweza ukahisi mie napita tu.. kwakusahau mie nina-hustle/
Nimezaliwa Afrika.. ugumu wa maisha umenifunza ku-struggle/
Ukiwa idle.. unamu-attract shaytwan (SHETANI)/
Kichwani nina MSAHAFU na BIBLE.. life ni zaidi ya ku-have fun/
Kwani.. Kila kicheche anajiona ni mzima/
Na njia pekee ya kuepuka ngoma ni kugoma kupima/
Ikiwa maujuzi haya hayakugusi.. itanilazimu nikuelewe/
Sometimes hata kamusi.. huimiss tafsiri yenyewe/
Nalindwa na dua za mama.. tangu baba simjui/
Namfanya adui mwenye njama aache drama na akue/
Ili ajijue kabla hajakwama huko mrama asitue/
Ajikwamue kwenye lawama.. yenye maana yamchukue/
Kisha anaiombee mimi ili nifaidike kwa hizi mbio/
Siamini kwenye umasikini hivyo sihofii mafanikio/
Ndiyo.. mie ni LEO kwahiyo sifikirii kushindwa/
Zingatia kauli hiyo hausikii inaashiria ubingwa?/
Mie ni mbishi.. muulize Nikki – hatopinga/
Na hata kama ningekua mbuzi ningelala chaka la simba

roho by fid q ft christian bella

(VERSE 1:FID Q)
Nilipommiss Hakutokea, ili kunigea kiss au kuni-hug/
Hakuni-care huyu binti, aliendelea kunimwaga/
Sijawahi penda kama hivi lakini mapenzi yakaniditch/
Nilisurvive vipi sikumuita 1st LOVE B@#$?/
Ninahisi.. nilipata vibe ya kuipa truth a facelift/
‘Haupati love bila michuzi hauna cash Fid ‘/
Nikakesha ndani ya booth.. HUYU NA YULE ikawa 1st hit/
Show kila mkoa haikosi groupie kwa guest list/
Life ikawa poa.. lakini u-Playa siuwezi Fid/
Sikufichi inaboa ile mbaya kuvaa jezi nyingi/
plus.. hawara anapasha kitanda moto/
Na haifanyi upweke ukaniacha kiasi cha kumganda huyu mtoto/
Na kuimba mahaba niue.. with a smile on my face/
Haijalishi kama ana uzuri wa kumturn hadi Gay straight/
Mapenzi ni kama ‘ ligi ya mbuzi ‘ Striker anaweza potea/
Wengi wanawa-cheat na kuwaudhi wachache wanao-Play fair/


CHORUS ( CHRISTIAN BELLA )
Mapenzi ni matamu lakini ninahofia kuumizwa moyo/
Nashindwa kujaribu.. roho inaniuma/
roho inaniuma x 5

BRIDGE ( CHRISTIAN BELLA )
Ninahofia.. kuumizwa moyo, bila hata kupewa pole/
dudu liumalo, kwanini nilipe kidole?/
ooh moyo.. roho inaniuma mie/

VERSE2 ( FID Q)
Dear hustle.. ni wazi penzi lako ni safi na huniacha happy kila wakati kubaki nawe ni kisamati baby/
Kipi sipati? ninahiti kwa chati.. waliotashtiti mziki haunilipi.. wako wapi? waniache.. mkate nipate baby/
Money makes a man.. lakini love ni hustle/
You know who you love but you dont know who love’s you/
Wakuniletea Baraka kama Michelle/
Na Tabasamu zaidi ya wafungua mlango wa 5 star hotel/
Dawa sio chungu ndugu.. chungu maradhi/
Hakyamungu tena.. chuki humchoma anayeihifadhi/
Kumsahau siwezi.. ni sawa na kumkumbuka nisiyemjua/
Mapenzi yalifanya nikaumbuka.. ninachoshukuru hayakuniua


CHORUS ( CHRISTIAN BELLA )
Mapenzi ni matamu lakini ninahofia kuumizwa moyo/
Nashindwa kujaribu.. roho inaniuma/
roho inaniuma x 5

sumu by Fid Q

[Verse I:]
Aliyeniumba alinipa mdomo hivo nina haki kuongea
Hii bahati meotea, safi kamwe siachi kui-share
Hamtaki niwe fair, trust me man huwa happy nki-care
Naona watachosema mshkaji uko smart upstairs
Usiache kuongea, usiache we ni incharge huna spare
Kipaji ka' Ngwair, mapaji ka' bahati aliowagea
Flag pepea, hitaji zaidi ya maji na mmea
Ilikuwaje wa muache hadi mshkaji ulaji wa drugs ukamzoea
Tunamoka ili kusafiri kihisia
Au kufoka pia ikitoka ukaisikia huwezi toka au ukitose kuingia
Kinachochosha nia, ni kosa ulichojua utapatia
Nawachota kihisia, nasota, je inatosha fidia
Shibe ya mdau hainilazi njaa sababu mganga yupo juu
Nafurahi ambavyo wadau wakimuona star wanalamba miguu
Asiye nihitaji simuhitaji, kamwe simuachi aje azinzi
Bandidu kama tsotsi sipigi goti ka' PNC
Hakuna ambae hakosi, labda kwa
Yangu self esteem haitoki ka' ripoti za TMZ
Na hainizuii nsile mkate, kwa kuhofia kiungulia
Na u-Emcee hauniachi, huniangalia ka
Ka' Bruce Lee hizi karate, ntakupigia utaishia
Na sinto sita kusema ahsante au kuwasifia mkinisaidia
Washkaji baadhi hawana haki ya kui-pressure hii medulla
Wako radhi kukupa pombe na siyo pesa ya kula
Nawaona vyura tu kama Snura, hii sura ya mhuni haina kwere
massawe anavaa suti mtaani, nyumbani kunguni tele
Kwa magonjwa yanayotibika tunapoteza maisha, Huruma
Tunachanga kwenye msiba ukifa, hawajali ukiumwa
Au wanaweza wakahisi umekufa kwa kukutwa umezirai
Usipo sh'tuka Afrika unaweza kuzikwa ukiwa hai

[Hook:]
Sumu
Sumu, Sumu
Sumu
Sumu,Sumu

trumpet plays...
[Verse II:]
Haumuui chura kwa kumtupa ndani ya maji
Ukinizuga kwa ulaji, nakupa fact kwa lugha ya kishkaji
Unataka vitu rahisi, mi' nawapa vitu halisi
Utata unamtaka ibilisi, na siyo bi kaka ka' Idris
Mr. Nice jua la utosi na mtaa unakiu ile mbaya
Hawamsupport, isipokuwa anawapromote aliowa-inspire
Wakati,sio kama Mox, Stosh hakupaswa kumgwaya
Lakini, mzee bila noti ni zaidi ya Nyoshi akiwa vibaya
I didn't come this far, just to come this far
Siwezi sanda kama bikra hata nikiishi ki-star
Maisha hayakupi unachotaka ila yanakupa unachotafuta
Pesa sadaka, wazushi wanaivuta kwa
Binadamu wako wapi mnanitoa mie nsiwemo
Leo nawapa ofa ya mswaki afu kesho mnaning'oa meno
Oyoooo.. time is money nafasi haijali kuzuga
Wema anataka saa ya almasi zari anaujali muda
Washa sana nyasi, rasta ogopa fast futa
Wanashindwa kujinafasi kwa unafiki nafsi zinawasuta
Wabongo wa majuu hamna upendo, mnajigawa
Ubongo hauna miguu lakini skendo zina mabawa
Aliyemtia umasikini Afrika leo analia kwa yanayomsibu
Na hutangaza akimpa msaada kiasi cha kumtia aibu
Dunia siyo chafu ni chafu uchafu tukiutazama
Sumu ndani ya watu, na ndiyo hapohapo tunapokwama
Hawaamini kwenye kuunda Diamond au Kiba wawili
Wanachoamini ni kumshusha mmoja ili mmoja awe dili
Cha kupewa hakishibishi ukipewa lazima ukumbushwe
Dunia mwendo wa ngisi, kung'aa sio lazima star ashushwe
Ukiacha hisia zikuendeshe, kwa ujeuri utaishia kufeli
Sababu neno la ukweli sio zuri na neno zuri halina ukweli
Ntasahau vyote, milele ntamkumbuka aliyeniumba
Na daily ntakaa mkao wa pusha tu kama Umbwa

bongo hiphop by Fid Q ft Majani

VERSE 1:
Ulianza wewe.. wakaja waimbaji na wabana pua
Wale mwewe.. Franga wawindaji wakatusua
Kwakuwa.. wanajua mshikaji unaishi kwa miko
na zako itikadi.. ziko kimziki na sio mshiko
Kama haileti hela..basi haimake sense.. no sweat kisela mie nikakomaa tu na lako penzi
Sikusound garbage au kuchange suddenly..
Mie ni mjeshi so naweza fight savagely
Hiphop ya ukweli.. ukapigwa radioni/sometimes malaika wa heri nao hutembelea motoni
Penzi ni kipofu na anayemuona halioni
sikuwa na hofu.. mama alinipenda tangu nikiwa tumboni
I started young.. I made my mother's womb a drum
My umblirical chord a guitar.. muhoji aliyenizaa
BONGOFLAVA mzuri kiasi.. hiphop we ndo my queen
my 1st.. my last & everything in betweenjj
 
Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time
Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2
 

VERSE 2:
Kama kukupenda wewe ni dhambi.. basi shetani yu nami
na kamwe sintonyea kambi ili niwabambe dukani
For a million little pieces naweza kumcon Oprah ka James Frey
Na watasema sitishi wakati wanaogopa nisitokee
Waufuate mkumbo huu wa wasomi.. wa midundo na mistari
ukiwa na nyundo mkononi.. ni rahisi kupigilia msumari
Sio tu bongo.. mpaka Ng'ambo hakuna uhuru wa habari
 kuna uhuru wa mwenye chombo.. mitambo na mwenye mali
Kujifanya hawasikii.. haiwasaidii.. wala haiwajengi
unachosema ni.. kamwe IPP haitompinga Mengi
Unawakumbusha wazazi wa uswazi.. chati ya uteja imeingia
na Mapusha wanauza drugs ili walishe familia
Mbaya.. kuhifadhi fuvu la mtu ndani ya kabati
mbaya zaidi ni kuwa na ndugu.. halafu kichwa maji
Amka bongo lala.. hiphop sio ufala.. ni lazima uifate
Uaminifu ni kama mshahara.. fanya kazi ili uupate

Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time
Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2

VERSE 3:
Mapenzi ya sikuhizi.. bila kugombana yanakua hayana stimu
Pia ni ruksa kushikana lakini sio kushikiana simu
Inanipa wazimu.. kusikia kimwana haujaachana na Hasheem
Na bado mnawasiliana..una mpango wa kuchanganya timu?
Nakupenda hiphop.. ndo maana ninarap ile mbaya
Naspit fire bila hennessy.. au kula kaya
I want my art to be my legacy.. kabla sijaretire.. waanze nigwaya hawa enemies.. anyways NI HAYO TU
Beef huletwa na wivu.. na wivu sio hiphop

siri ya mchezo by Fid Q ft Juma Nature

(verse1):Fid Q
Nilipotoka mbali na ninaheshimu nilipo
sikuwa na  umuhimu kihivyo
stimu  zikanipa elimu ya Biko
Kimaandiko
kimistari..
hadi fans wanascream nikirap
sikuamini kama nina zali mpaka nilipoidream hiphop
Wanapagawa…. Na baadhi ya mambo nayoyajua
pia nina uwezo wa kufanya mpaka madawa yanaugua
Wanapagawa na nyimbo ngumu hawa  #teamMabiiitoz
Achana na  power window.. sijui  rimz za dimpo 
haileti bingo, mshiko?  Star ishi simple
sanaa iko hivyo sometimes.. hukataa kukaaa ulipo
wanaodharau.. hujiletea matatizo..hawajui  kama
wadau hupendelea kukuona hivyo
bonge la staa.. donge la njaa.. hauna kitu
jikombe ugongwe…mtaaa  ukuone hauna ishu
ukishindwa kujiandaa… jiandae kushindwa
mjinga utaachwa unashangaa kumuona Martin Kadinda
Usmati anaotinga, majumba mandinga ya bwana Almasi
je hizi track za  harakati ni ujinga
HAPANA…. nguvu ya mamba ni maji
na umaarufu au kutamba.. kushika namba ni bahati..
sio kipaji  kama  Kubanda eti unachana kigumu
kisa  track ikivuma sana kwenye chati  haidumu
Amani kwa chachage na MAKUWADI wa SOKO HURIA.
baba asante kwa UTAFITI na ZAWADI ya ALMASI ya BANDIA
NYUMBANI… nasikiliza DUNIA YA SASA ya MARIJAN 
najiuliza tutarithi nini ikiwa IMANI ishakwisha tangu zamani
labda kubisha na wakinitisha najihami
inasikitisha unapoibiwa na aliyekupigisha ni jirani
 ‘’ Pole MAPROSOO’’ uhujumu –uchumi umefanya umetubu
WAZEE ni  wahuni  hadi soo waay back before SUGU
Taifa la kondoo.. huendeshwa na serikali ya Dubu
na MBWA MWITU wenye siri.. ili bepari umuabudu
kimahakama, kiserikali, kidini umsujudu
huo ni utumwa pia
Unafanya  vijana  wanaumia.
Tunaishia kufia mabatani kama nzi ndani ya glass ya bia


CHORUS:  ( Juma Nature )
Siri ya mtungi aijuaye kata
komaa… kaza.. kisha utapata
Siri ya mtungi aijuaye kata
komaa… kaza.. kisha utapata
Siri ya mchezo naijua  mimi
tu.. na hakuna mwingine
Siri ya mchezo naijua  mimi
tu.. na hakuna mwingine

(Verse 2):Fid Q
Tofauti ya BIASHARA na SIASA ikila hasara inaweza buma
wakati SIASA kila mara ukiwa unang’ara ujue kuna
kinara anayeunda msafara wa wanaojituma na
kuchuma kwa kukufanya uwe imara hapo hasara hakuna
KIDUMU CHAMA CHA MASELA…
Ukoloni mambo leo umetupa uhuru wa bendera
tuone kufuru za wenye hela
TANZANIA ni ‘  demu wa mtungo ‘ wanamuiita CHA WOOTE’’
HANGOVER .. ‘’anaikimbia kwa kupiga ‘ “ mtungi “ saa zote
Mkubwa anazuga atasolve… matatizo ya nchi yake
‘’na  gari bovu..’’  halisukumwi kwa kukaa ndani yake
MAENDELEO ni ile ndoto..MWEZEKAJI ashaipuuza 
je  Kukaa karibu na moto ni kuuota au kujiunguza
hakuna UHURU wa kweli (Africa) msidanganywe na illusion
na daily tunafeli sababu ya  POLITICAL institutions
CIVILIZATION  imeadvance sasa wanatuua economically
hakuna utumwa mbaya kama ule wa kujiona uko free
Kuusaka ukweli  ni  sawa na kumenya kitunguu
kila ganda litakutoa machozi na utabaki macho juu
Ukishafika kwenye kiini  niambie nini utagundua
zaidi ya mafaili yaliyounganika utaghairi kuyafunua
Wamejivisha U-NOAH.. SAFINA zao zikatoboka
Wakajivisha U-MUSSA.. FIMBO zao hazikugeuka NYOKA
sasa wanaujaribu Umungu mtu kuamua leo nani atatoka

CHORUS:  ( Juma Nature )
Siri ya mtungi aijuaye kata
komaa… kaza.. kisha utapata
Siri ya mtungi aijuaye kata
komaa… kaza.. kisha utapata
Siri ya mchezo naijua  mimi
tu.. na hakuna mwingine
Siri ya mchezo naijua  mimi
tu.. na hakuna mwingine

sihitaji marafiki lyrics by Fid Q ft Vyonne Mwale

   
CHORUS
Machizi sikusoma nao, tulikutana tu mtaani
 udogoni sikucheza nao lakini ndo machizi wa ukubwani
Machizi sikusoma nao, tulikutana tu mtaani
udogoni sikucheza nao lakini ndo machizi wa ukubwani


VERSE1
haijalishi ulikua na wangapi bali wangapi uko nao
..washkaji ambao... kosa lako lao wakati hauna mafao/wanaokufikiria wewe muda ambao/ wenzao walionao wanafikiria wengine ndo wanao/now
kupata washkaji ukiwa na pesa... ni rahisi/
kuwapata na hauna kitu ujue umefanikiwa kichizi mie sikufichi sihitaji urafiki na usupastaa/ukihit ndo unang'aa.. upishwe useat kwenye bar,upewe beat na Jr../ kitu ambacho haikuwa rahisi kipindi fid ni underground/sikuhizi mabinti wanaomiss ni walionidiss mie sio mdau/
wanakubali mie ni mkali wanataka kuijua Mmwanza
ninayoitangaza nikiwa safari kama habari za kwanza/
U-N-I-T na prof Ludi walionifunza kukaza...
kwetu mbali.. sijui lini nitarudi? (C) Lokua kanza/
sihitaji marafiki, labda baadaye wakitokea/aje mmoja wa kuongea nae, na mwingine wa kumuongelea

CHORUS
Machizi sikusoma nao, tulikutana tu mtaani
udogoni sikucheza nao lakini ndo machizi wa ukubwani
Machizi sikusoma nao, tulikutana tu mtaani
udogoni sikucheza nao lakini ndo machizi wa ukubwani

 
VERSE 2;
na usupastaa huwa ni feki.. utakung'arisha ukiwa na Market/
utakupatia senti,utapita juu ya red carpet/
utageuka young & restless, utakupa wanawake/utakupa mafake brethrenz.. kisha utaenda zake/kwahiyo power its not permanent.. huwa ipo kwa muda tu/respect ur own conglomorete... fikiri kikubwa tu/masaa hayarudi nyuma kama muda wa kufuturu walioukataa utumwa wanastuka hawana uhuru/
wanazusha najiskia.. so im my own best friend/
sikia fidq anamsifia fareed ni bandidu sio Yes man/
naweza nikakata ringi kiasi cha kutopay attention, lakini sio tajiri wakuafford kuua true friendship/
tuweke siasa kando sababu kichwa kinanigonga/na hizi falsafa double double ajabu sio kinywa cha mjomba/
sihitaji marafiki, labda baadaye wakitokea/aje mmoja wa kuongea nae, na mwingine wa kumuongelea

CHORUS
Machizi sikusoma nao, tulikutana tu mtaani
udogoni sikucheza nao lakini ndo machizi wa ukubwani
Machizi sikusoma nao, tulikutana tu mtaani
udogoni sikucheza nao lakini ndo machizi wa ukubwani

VERSE 3
rafiki wa kweli yukoje.. ni mkimya au anayechonga/yule aliyekupa jina?au pengine anayekuponda? anayezuia usidondoke au anayesubiria kukuokota?/au ni yule ambaye ukimuudhi anakutusi kabla hajaondoka?/ hakuna adui mbaya ka rafiki yako mwenyewe ambaye hajui.. ka yupo nawe.. au yupo kinyume na wewe/bora adui.. kama hachachawi utaenda muomba akuelewe/
ka buibui.. naweka tandu mtaenda kando mzingue?/
kwani machizi wenyewe wako wapi ambao wanastahiki niwape vyeo/ inabidi tu uwaache wakuwatch kwenye kideo/unakula nao happy leo.. kesho wanamtaka mkeo/urafiki sitaki.. hauletagi maendeleo../
nilitamani kuwa mjamaa niwe genge kama nature/
wachache niliowafanya wakang'aa wanayaweka maisha yangu in danger/
sihitaji marafiki, labda baadaye wakitokea/aje mmoja wa kuongea nae, na mwingine wa kumuongelea