ningekusamehe lyrics by 20%


uliponitosa mie, nilibembeleza ukataa tena..
sikuwa na kosa mie, mie nahisi sina chapaa
sasa sijapata, hata kama nikipata
nitazidi kutafuta, naomba ondoka
mwenye mapenzi ya kweli, asije akakuta

ningekusamehe ila, ila wewe huna ila
ningekuwa na we, ila, ila unapenda sana hela
eeh

nani? alotaka kunitoa roho, penzi likafika mwisho
mimi, ya kale achana nayo, niko chini ya miguu yako
kwani nani? alotaka kunitoa roho, penzi likafika mwisho
mimi, ya kale achana nayo, niko chini ya miguu yako

mmh
mhhh

basi sikia mpenzi, mbona wanipa kazi
bila wewe siwezi, nitajawa na simanzi
mwenyewe wajua, jinsi gani nimekufia
basi nakuimbia, usiweze kunikimbia
unajua sina ujanja wa kuachana nawe
kuniacha njia panda, nitapata kiwewe
huyo mtimue, mi unirudie eh
usiniache nilie, wewe ni wangu mie
mhhh, eeeh

ningekusamehe ila tayari mi nishampata mwingine
ulitaka uniuwe nitaichwa chizi mi nikikupa nafasi nyingine

nani? alotaka kunitoa roho, penzi likafika mwisho
mimi, ya kale achana nayo, niko chini ya miguu yako
kwani nani? alotaka kunitoa roho, penzi likafika mwisho
mimi, ya kale achana nayo, niko chini ya miguu yako

ni machungu kiasi gani, uliponiacha gizani mi
ulitaka nifanye nini, kama si kusaka kampani
nilidata, nikasaka, na hatimaye nikapata
nashangaa, wanifuata, eti tusahau yalopita

ningekusamehe ila ila, ila sio kimapenzi
ningekuwa na wewe ila ila ila nimeshapata mupenzi

sina habari, sitaki kuwa nawe tena
huna nafasi ndo hivyo nishakutema
nakupa fact unielewe kiundani
sina mapenzi kwako yalikuwepo tu zamani
nenda tu uniache wala usijali
nimempata mwingine ananipa mapenzi ya kweli
ulivyonitenda mi nasema iliniuma
we nenda tu mi sikutaki tena
sina habari mami sikuhitaji tena
mtoto mzuri nipo naye mwenye heshima
na shida zote atavumilia na
atanipa mapenzi ndivyo alivyoniambia
andika story ya kwamba ulikuwa nami
andika story ya kwamba ulikuwa nami
kifo cha panzi ni furaha kwa kunguru
sikutaki tena mami we niache huru

nani? alotaka kunitoa roho, penzi likafika mwisho
kwani nani? alotaka kunitoa roho, penzi likafika mwisho


No comments:

Post a Comment