siachani nawe by Baraka da Prince

(verse1)
Wakati nalainisha moyo kupenda sio kama ninakosea
ipo sababu ya mimi kurejesha namba ambayo ilipotea
hali ya mtoto kumsusa mama akishachapwa
ni sawa na mapenzi
ukishapendwa
unasahau hata kama ulishafanyiwaga ushenzi
nakumbuka nilijuta sana kupenda kupenda kusikokua na thamani
ila hitaji la moyo lalazimisha kurudia zamani 


(chorus)
mimi bado nina imani
ipo siku utanipa thamani
mimi bado nina imani
jua me siachani nawe
na sishindani nawe
maana upo moyoni ndani
acha nisote mie
ila me siachani nawe
na sishindani nawe
maana upo moyoni ndani
wacha nisote mie

(verse2)
labda juu ya kaburi utanipenda mimi nikiwa sina uhai
hisia zangu haziheshimiwi najidharau sifai
heri ya upofu wa macho
kwa yale nayoyaona
umeruhusu mboni zangu me kumwaga machozi
yaani ungejua hisia za mapenzi
kutesa moyo ila bado hazichoshi
kupendwa sipendwi najua wazi ila bado silingi
maana kesho nitaurubuni moyo
unapendwa na unapenda me meno ila najiona kibogoyo
kweli penzi donda moyo

(chorus)
mimi bado nina imani
ipo siku utanipa thamani
mimi bado nina imani
jua me siachani nawe
na sishindani nawe
maana upo moyoni ndani
acha nisote mie
ila me siachani nawe
na sishindani nawe
maana upo moyoni ndani
wacha nisote mie