I'm sorry JK by Nikki Mbishi

(Chorus)
It will one day make sense/
Nikisema hakuna president kama JK/
Tanzania inakumiss yaani daily/
Kwa niaba ya wabongo I’M SORRY JK/ (x2)

(Verse1)
I’m sorry JK nimeona tu niseme/
Mzuka huu niliupata nikiwa Juu Kijenge/
Mikopo hakuna tena huendi chuo kikuu kizembe/
Bungeni wanalewa wanabonga tu king’eng’e/
Wakitwanga wanatamba wakisanda wanatubu/
Simuoni tena Jay tangu akutane Sugu/
Scorpion amegeuka ghostface mwema/
Aliyeota Rais atakufa anaitwa Godbless Lema/
RC na Wasafi uswazi madefender/
Hapa Kazi tu mtaani njaa kali sio sinema/
Kama kuisoma tushaisoma namba/Ungegombea awamu ya tatu ingekuwa bora labda/

(Chorus)
It will one day make sense/
Nikisema hakuna president kama JK/
Tanzania inakumiss yaani daily/
Kwa niaba ya wabongo I’M SORRY JK/ (x2)

(verse2)
Enzi za bibi cheka wengi walikuita babu cheka/
Hawakujua kuwa nyakati zinakuja nakusepa/
Ulivunga wakibeza kuwa unapenda sana bata/
Na kiki ka” Makonda za Wasafi kuwafuata/
Wabongo watakumbuka kwenye sekta ya michezo/
Mpaka Taifa Stars nayo ikaonesha mauwezo/
Ukaongeza vigezo nyenzo matengenezo/
Leo Samatta ndo kinara na hachezi soka la dezo/
Tuzungumze magazeti Bunge wanaedit/
Hakuna mikakati bwana kumbe wanaekti/
Demokrasia demoghasia za Field Force/
Wengi wanafear ukweli kuwaambia Unju siogopi/
Mabenki yanafilisika madeni yanamimika/
Hali imekuwa ngumu hadi wageni wanasikitika/
Hatusheshi na shisha yaani sio fresh inatisha/
Bar mwisho saa sita siku hizi hatukeshi kabisa/

(Chorus)
It will one day make sense/
Nikisema hakuna president kama JK/
Tanzania inakumiss yaani daily/
Kwa niaba ya wabongo I’M SORRY JK/ (x2)

(Verse3)
Kila taarifa ya habari leo JPM/
Pesa imepotea kimazingara David Blaine/
Waathirika hawaelewi juu ya mipango ya Bukoba/
Tetemeko wasije kula michango ya Msoga/
Tumekosa usitupe laana tucorrect/
Weka kando chama tuwe wana tuconnect/
Hela imefichwa nyuma ya Pazia la viwanda/
Njoo Sogodo uone Tanzania ya vibanda/
Uone chafu moja na askari mia wakisanda/
Chocho za Panya Road mixer pwiya la miganja/
Kuna nyakati nilikudiss JK/
Now I’m calling for the peace,DAMN! We miss JK/
By Nikki Mbishi 2016

dume suruali by Mwana Fa

we ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami
kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami

(verse1):MwanaFa
who dat who dat hii ni salam na ufahamu
Kama unauza mapenzi sio kwa binam
Hakuna haja ya kusubiri hii ni hukumu
Hakuna kitu utapata utangoja kama askari wa zamu
Dume suruali Dume kaptula
Shauri zako mradi sipati hasara
Usione utani me sihongi hata kwa ishara
Utaniambia nini mpaka unigeuze fala
Kwanza nasikia hongo zinaleta mkosi
Sentano yangu hugusi Hata ukiongea kidosi
Yabaki mapenzi tusileteane ujambazi
Hata upige sarakasi Utachonga Viazi

(bahili kama nini!!!!!!)

Ndio mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

(Chorus):Vanessa Mdee
we ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami
kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami
i want that gucci fendi
spend all on a girl like me
my name is vee money money
spend all on a girl like me

(Verse2):MwanaFa
Nihonge nanunua nini kwanini yani
Kuna kipi nisichokijua ina TV ndani
Usiulize ntakupa nini dada piga moyo konde
Viuno vingi kama mwali wa kimakonde
Usipende hela kama mfuko
Au fanya unavyofanya upate zako
Vishawishi vingi binti sema na moyo wako
Na ujifunze pesa zinauza utu wako
Tajiri mtata kama Salah
Zipo ila sitoi me ni balaa
Unapenda hela zangu nami nazipenda pia
Kila mtu abaki na zake bye baby tutaongea

(mwanaume wa hivyo wa nini sasa!!!!!!!!)

Ndio mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

(Chorus):Vanessa Mdee
we ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami
kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami
i want that gucci fendi
spend all on a girl like me
my name is vee money money
spend all on a girl like me
(Bridge)Vanessa Mdee
Aje aje ajeeee Me mtoto fulani ghali
Nihonge gari Ma swt swt baby
i wanna C u to day unipeleke party
Aje aje ajeee Njoo nikupe TBT

(Verse3):MwanaFA
Sio kwa enzi ya Magufuli
Zali ilikuwa long siku hizi hakuna la mentali
Nikikuhonga na ukiniacha nitakujia usingizini
Naepusha shari matatizo yote ya nini
Hakuna kipya chini ya jua
Hata nisiyoyafanya nishayasikia
Ningekuwa mhongaji ningeshafulia wangu
Mademu wangu wa zamani wote wangekuwa maadui zangu

(mwanaume ovyo wewe!!!!!)

Ndio mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisifii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

(Baki na hamu zako

(Chorus):Vanessa Mdee
we ni dume suruali kaa mbali nami, mbali nami
kama dume suruali kaa mbali nami, uendani nami
i want that gucci fendi
spend all on a girl like me
my name is vee money money
spend all on a girl like me
(baba bure huyu)

Hata pantoni lina staff

unamwambia nani sasa
unamwambia nani sasa