I'm sorry JK by Nikki Mbishi

(Chorus)
It will one day make sense/
Nikisema hakuna president kama JK/
Tanzania inakumiss yaani daily/
Kwa niaba ya wabongo I’M SORRY JK/ (x2)

(Verse1)
I’m sorry JK nimeona tu niseme/
Mzuka huu niliupata nikiwa Juu Kijenge/
Mikopo hakuna tena huendi chuo kikuu kizembe/
Bungeni wanalewa wanabonga tu king’eng’e/
Wakitwanga wanatamba wakisanda wanatubu/
Simuoni tena Jay tangu akutane Sugu/
Scorpion amegeuka ghostface mwema/
Aliyeota Rais atakufa anaitwa Godbless Lema/
RC na Wasafi uswazi madefender/
Hapa Kazi tu mtaani njaa kali sio sinema/
Kama kuisoma tushaisoma namba/Ungegombea awamu ya tatu ingekuwa bora labda/

(Chorus)
It will one day make sense/
Nikisema hakuna president kama JK/
Tanzania inakumiss yaani daily/
Kwa niaba ya wabongo I’M SORRY JK/ (x2)

(verse2)
Enzi za bibi cheka wengi walikuita babu cheka/
Hawakujua kuwa nyakati zinakuja nakusepa/
Ulivunga wakibeza kuwa unapenda sana bata/
Na kiki ka” Makonda za Wasafi kuwafuata/
Wabongo watakumbuka kwenye sekta ya michezo/
Mpaka Taifa Stars nayo ikaonesha mauwezo/
Ukaongeza vigezo nyenzo matengenezo/
Leo Samatta ndo kinara na hachezi soka la dezo/
Tuzungumze magazeti Bunge wanaedit/
Hakuna mikakati bwana kumbe wanaekti/
Demokrasia demoghasia za Field Force/
Wengi wanafear ukweli kuwaambia Unju siogopi/
Mabenki yanafilisika madeni yanamimika/
Hali imekuwa ngumu hadi wageni wanasikitika/
Hatusheshi na shisha yaani sio fresh inatisha/
Bar mwisho saa sita siku hizi hatukeshi kabisa/

(Chorus)
It will one day make sense/
Nikisema hakuna president kama JK/
Tanzania inakumiss yaani daily/
Kwa niaba ya wabongo I’M SORRY JK/ (x2)

(Verse3)
Kila taarifa ya habari leo JPM/
Pesa imepotea kimazingara David Blaine/
Waathirika hawaelewi juu ya mipango ya Bukoba/
Tetemeko wasije kula michango ya Msoga/
Tumekosa usitupe laana tucorrect/
Weka kando chama tuwe wana tuconnect/
Hela imefichwa nyuma ya Pazia la viwanda/
Njoo Sogodo uone Tanzania ya vibanda/
Uone chafu moja na askari mia wakisanda/
Chocho za Panya Road mixer pwiya la miganja/
Kuna nyakati nilikudiss JK/
Now I’m calling for the peace,DAMN! We miss JK/
By Nikki Mbishi 2016

No comments:

Post a Comment