Ukisikia Paa lyrics - JCB ft Fid Q, Chidi Benz

 ahhh...ahhhh
 ohhh yeahhh..(shhhh!).. it\'s the remix
 (shhhh!)...JCB.... (ahhhh!).....Murder..!
 (Tongwe Records Babyyyy)

 Verse 1 (JCB)
 Damu ilitapakaa baada ya ule mlio kulia PAAA,
 Watu wote walisambaa hata walevi wa kwenye bar,
 Sio polisi sio baunsa iliye kaa utashanga kwa nini mshkaji alizidi kumimina kwa kujiamini,
 Amini usiamini akabaki tu na mimi,
 Akanishikia bunduki kwa chini,
 Akadai eti nimpe madini lasivyo ananipiga risasi kama sabini,
 Anasura kama idi amini akarudi karibu atua tatu mpaka kabatini,
 Akatamka HEYOO! nipo kazini nimetumwa mzigo au ujithamini,
 Akanikanyaga kwa chini kikorofi bunduki tena akaikoki
 Akasema kama simuonyeshi leo sio koki,jinsi alivyo akilenge ye akosi mikosi,
 Kavaa koti jeusi jasusi,
 Mikono nikaweka juu kuepuka nukx huku natukana mengi matusi...

 (Chorus )
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
*2

 Verse 2 (Fid Q)
 Wanasema hugeuka mnyama sana anaposaka pesa
 Cha ajabu anavuta bangi lakini hawazii magangstar
 Hampaki rangi donkey ili ageuke kuwa zebra
 Ndo maana kabla hajaikoki, JCB ali-surrender
 Akajifanya hayuko na mie ili niipigie defender
 Nikaona vipi nijistukie ghafla nikasikia \'\'RASTA\'\'
 Jambazi linaniita halafu sioni wakuni-backup
 Hali inatisha sikuongea nilishut the fluck up
 Akaniuliza.. we sio Fid Q yule anayeheshimika mtaani ?
 Nikamwambia ndo mimi na huu ndo muda wa kumlaani shetani
 Sie wote ni watoto wa mjini siamini vipi hatujuani
 Mie alwatani kama Kwere au Chindo popote amani
 Akaniambia.. waambie machizi i\'m sorry, leo mna-rap wapi ?
 Mie sio mtu wa stories, i make things happen
 Hii sanaa ni ya watengwa na ngosha...
 Ukisikia Paaaaaaaa........ ujue imekukosa

 (Chorus)
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa

 Verse 3 (Jay Moe)
 (aahhh!) Alipogundua ni wasanii,haraka haraka akatuacha
 Ndipo tulipomsihi,na watu wengine kuwaacha
 Maana ishakuwa msala,na mashahidi nyuzi washavuta
 So muda wowote defender,toka hivi sasa itafika
 Bora usepe..kuliko kupewa kesi ya mauaji
 Au kesi ya kujaribu,kupora kwa kutumia mkwaju
 Hakuna mwenye mzigo,waambie wenzako mme-boogie
 Na wala hatuna kimango,usione mezani kinywaji
 Achana na mambo ya leo,wapi tunapiga show
 Pigia wenzako simu,waambie huku ni soo
 Hakuna mtu wa madini,sema ni kina jaymoe
 Kabla haujaishia mikononi,kwa gorvo..au you know !
 Ile anaanza kuchomoka tu,polisi washawasili
 Nikasikia mikono juu..kwa sauti ya ukali
 Kukimbia akala ya mguu,akasalimu amri
 Akanyoosha mikono juu

 Chorus
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
*2
 Verse 4 (Chidi Benz)
 Hata police ni mdili na ndo mchongo ameupanga..
 Na ndo yeye wamemtuma jukumu lake kuwa mwanga...
 na ile paaahh!! Kama Suka kama kulenga mchanga
 Mwisho wa siku mahesabu watu wakacheze fanga
 Mchezo kamili ulishapangwa yaliyopita ni historia...
 na maneno kaa ya kwenye kanga ya hesabu nishatulia
 Wa kucheka wamecheka wa kulia wamelia
 Nchi bado haikufea so hamtochoka kusikia
 Michezo kama hii kurudia ninajua walala hoi
 Wamechoka vumilia...yeeahh
 Damu zitamwagika kwa wema na wasio wema...
 na imani ya mkabaji ulichokimeza utakitema
 Kuna movie ila maisha ka cinema
 Unyang\'anyi na uchukuzi unaoatokeo kila nikihema ...(hema)
 Wanasema ukila nyama....lazima utake tena..
 na kweli macho kwa maneno ya viongozi wanaosema
 Ni vigumu kutumkia kabla tonge kuingia
 So anytime tuwe tayari kuumia....yeeahh
 Ni vigumu kutumkia kabla tonge kuingia
 So anytime tuwe tayari kuumia....yeeahh

 Chorus
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
 Ukisikia PAAAA...ujue imekukosa
 Aliyelenga hana shabaha...amefanya makosa
*2


4 comments:

  1. iko poa sana hiyo!kazi nzuri!

    ReplyDelete
  2. Hip-hop kali Sana hii. put in bongo hip-hop history By Abel Bukwimba Fro mwanza kiseke.

    ReplyDelete
  3. hatari sana hii ni hit song

    ReplyDelete