movie ya kwanza Peter Msechu kuigiza

cover ya hiyo movie



Hii ndio movie ya kwanza kuigiza mwimbaji staa wa TUSKER PROJECT FAME Peter Msechu, ambapo amelipwa shilingi milioni 2 za kitanzania kuuza sura yake na ujuzi humo ndani.

stori ni kwamba Wema Sepetu alinunua appartment ambayo aliekua anaimiliki zamani ndio alimpangishia Msechu lakini wakati anamuuzia Wema, hakumwambia Msechu kwamba nyumba inauzwa so ikafikia wakati Wema Sepetu akawa anafukuza wapangaji wote ili aifanyie nyumba Marekebisho.

Baada ya hapo wapangaji wote wanaondoka anabaki Msechu ambae anaigiza kama Mpangaji Mtukutu, sasa hapo ndio movie inaponoga.

Inatarajiwa kuwepo dukani kuanzia wiki ijayo.



source.milliardayo.com

No comments:

Post a Comment