Kichaa cha Mbwa by Nikki Mbishi

yeah haha, yeah yeah
you know who i be, toka lunduno
Yeah, Bongo Jnr, Shasho
Nikki Mbishi in the Building yeah yeah
Im Busy, Im Busy, Im Busy yeah
yeah, yeah

Nakuja moja kwa moja na sishtui kama Joti
Sipumui na troti, nakata wimbi zaidi ya Boti
Nipo kifedha zaidi chagua siimbi kata noti
kukopi huogopi, msamaha hautoki kwa magoti
ubongo kamwe hausimami, sawa na meli juu ya lami
treni nje ya reli mteni we umeshafeli mtihani
sehemu kama msibani huzuni usheeni mtimani
watani msikae karibu nami mtaitonesha amani
mvua imenyeshea godoro leo unalala juu ya chaga
hutaki sakafu ipo kazi kwako kujimwaga
msanifu, sanifu lugha wanaweka nawekaga
wakuja wanazuga, wanashangaaje wanataga
nimecheza legeza lakini sio big deal
mautundu nikayaongeza kwa kuweza ku'make it real
wake up nigga buni vya kwako usipende vya kuiga
nastaajabu kuona swala anatamani matawi ya twiga
ridiculous, street wanasema nikki ni dangerous
scandalous, flow nnazotema sio weak ni tremendous
mapaparazzi wa uswazi hawapakazi
maviwako nakazi kushusha ngazi siwakatazi whaat?

kichaa cha mbwa ni kama cha panya buku, cha panya buku, HEYA HEYA!
kichaa cha mbwa ni kama cha panya buku, cha panya buku, MZEIYA MZEIYA!

Hizi habari za kuamina si hadithi za kakakuona
ukifa unazikwa na kusahaulika ka Issa Matona
siku ikifika macho yataongea na mdomo utaona
ugonjwa utajivika sanda kwa kukata tamaa kupona
hii mistari itagusa kila mahali,
antenna nazo bila booster zitashika stesheni za mbali
wanaostaajabu ya Musa wata..
patwa na mshangao wa samsoni miamba nikiangusha
majabali ya mfalme faraoh, na...
sibumbi stori kuteka fikra za watu kama mtungi shauri ukishtuka
umekunwa mpaka viatu, sometimes nasmoke rolls za ganja kichwa kiwe fyatu
punguza chenga tafuta goli ***********
askari acha nijipange tayari kwa shambulizi, siulizi mtanange
kiafande silali usingizi hii ndo lifestyle nnayoishi ukinifwata utapotea
usishangae nnavoitwa mbishi afu naishi kwenye ghetto ka la gwair

kichaa cha mbwa ni kama cha panya buku, cha panya buku, HEYA HEYA!
kichaa cha mbwa ni kama cha panya buku, cha panya buku, MZEIYA MZEIYA!

Ni kama kawa biashara asubuhi jioni mahesabu
kiuchumi sjauawa dhiki sijui shida au taabu
nacheki usawa hakuna bedui, wote wastaarabu
wanapagawa nnavocheza na chui mwenye ghadhabu
ile ki'Gangsta, fegi mdomoni moshi hewani na drive Lexus
gold shingoni kiunoni gani mziki mzito
niko high speed road inachomwa heavy mkito
namuwahi waridi baridi so narudi ghetto
kuta machizi wameshajiri na wame'settle
toka longtime wanansubiri nawapa tano
freestyle za hapa na pale natoa michano wana'smile kwa mitindo ya kale
huyu, yupi mnene yupi ni.. choka mbaya
nipo kimapene wengi mifuko inapwaya
nafanya vile navopenda kwani bongo kama ulaya
maskani kama Jamaica kuna'smell ka ya kaya
nikki, Mbishi, kwa stiki, humtishi
natapika matapishi tumboni siyarudishi
fuatilia nyendo zangu mchimba chumvi utoke dry
bye-bye, mi nawahi na fly bad dont cry

kichaa cha mbwa ni kama cha panya buku, cha panya buku, HEYA HEYA!
kichaa cha mbwa ni kama cha panya buku, cha panya buku, MZEIYA MZEIYA!


ukinipenda shangwe, usiponipenda chukua time, niacheni mi niandike rhymes
Nikki Mbishi na Dunga wa Mandugu , MZEIYA MZEIYA
Kama hujui kitaa mamoshi busy, nalipresent toka lunduno Entertainme..
lazima waseme, wacheze kama sebeene, hahaha.. lets go..haha..yeah
MZEEIIYA MZEEIIYA

No comments:

Post a Comment