nikupe nini by Noorah ft Ali Kiba



Fish crub music
Ni baba k ali k once again

(verse1)
Nikikupenda unaanza niringia
Nikipunguza upendo unaanza nililia
Au ndo mwalimu wako kipofu
anakufunza kula mfupa palipo minofu
Kama bado unajali hujali we bado hujapata majibu nikuache ukatarii tu
Maana huachi kuaribu haribu vile kama unalisaka bifu
Tunapendana au tunapima au tunashindana
aah unachisana aah tunabishana aah
Umekuja kunipenda au uje kunitawala
Me mwenzio nakuheshimu ujue
 kama hupendi tunavyoenda tuvunje mkataba
Nijue moja nisijisumbue

(chorus)
Unapenda migogoro gogoro
Kila siku migogoro gogoro
Me na we migogoro
Ndani migogoro
Hivi nikupe nini ufurahi me na wewe twende sawa
Nimeshatapeli wajanja wa town nusu niende jela
Kila siku migogoro
(verse2)
Na masharo uwezo wanakula zaidi
Sijui ni utoto au uko ndio unafaidi
Unavyozidi kutumika thamani yako inashuka
Me ntaumia ntasikitika baadae sitakukumbuka
Nikiwa gentleman me bwege
 unajisifu eti ushanikamata eeh
Nikichange kwa bed me kicheche
Utaanza mapepe hadi wajinga watachapa
Unataka nikupe mapenzi hadi usiyoyahitaji
Au nikutumie kwa sex then nikudischarge
Sijui sisi ni wapenzi au maadui
Au labda mapenzi me ndio siyahitaji
Vitu vingapi nihuvipati
Sema Vitu vingapi si huvitaki
Mapema siku ni ngapi zimebaki kunitema
Jibu now usinigasi tena

(bridge:Ali Kiba)
Nikiwa na kosa unafoka foka
We ukiwa na kosa ndio tulivyoumbwa
Me nikiwa na kosa unatishia kuondoka
We ukiwa nakosa hata huna msamaha

(chorus)
Unapenda migogoro gogoro
Kila siku migogoro gogoro
Me na we migogoro
Ndani migogoro
Hivi nikupe nini ufurahi me na wewe twende sawa
Nimeshatapeli wajanja wa town nusu niende jela
Kila siku migogoro

Noorah a.k.a baba styles ali k

No comments:

Post a Comment