Kama zamani by Mwana FA ft Mandojo & domokaya & kilimanjaro band (njenje)


[Intro - Mwana FA]
Keeping the good music alive
Thats my job!
I like the way y'all lookin' tonight
Wow!
This is the..eer..kind of music you can twist up to
I mean like..er..to the left, to the right
Step it up, to the right, C'mon!
Left, right

[Hook - Dojo,Domo&FA]
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani (kama kama kama kama zamani)
Natamani iwe Eeh! (Lets Go!)
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani (kama kama kama kama zamani)
Natamani iwe Eeh!

[Verse 1 - Mwana FA]
(Feel me!)
Sikukukosea nilikukosea kuamua
Nkadhani umenikosea sana nkashindwa kuchagua
Machozi yangu na maumivu yana uhusiano unajua
Nawezafanya chochote rudi maa Mungu anajua
Bado sinywi pombe kama ulivyoniacha shuga
Huwa naswali ila sifungi mawazo yamenipa ulcers
Wananicheka ujinga 'coz nakuongelea wewe tu
Nikiongelea mapenzi mfano wangu wakwanza ni wewe boo
Kama ni ndoto naomba Mungu iishe mapema
Naona mateso ka' naibeba dunia nzima
Nashindwa kula nashindwa kulala mama
Kila kukicha naumia kama tuliachana jana
Ni jeuri tu zinaniumiza
Yasingefika huku kidume nisingeendekeza
Mara ngapi nilikosea mimi na ukanisamehe
Mara ngapi ungeweza kuliacha penzi lipotee
Hukuniacha ukaganda na mimi kama ulinizaa wewe
Nilishindwaje kusamehe wakati ulipokosea nawe!
Tungeachana usiku tukarudiana asubuhi
Jeuri tu zinaniongoza nashindwa hata kumsabahi

[Hook - Dojo,Domo&FA]
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani (kama kama kama kama zamani)
Natamani iwe Eeh! (Lets Go!)
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani (kama kama kama kama zamani)
Natamani iwe Eeh!

[Verse 2 - Mwana FA]
Siwaulizi shosti zako kama bado unanikumbuka
Siwezi majibu yao ya shombo yatanisuta na ntawachapa
Sijasahau walivyonibembeleza enzi tunavunjika
Na nilivyogoma kuwasikiliza wote vicheche nkawaita
Sikuwa na uwezo wa kuku-treat kama millionaire
Mapenzi yakazidiwa na maisha we had to break somewhere
Yes ulinikosea na ukanifanya nkalia
Nkashindwa kujikaza ikanibidi kukuachia
Hukuamini maneno yangu hukupenda the way they sounded
Au labda ahadi zangu hazikufikia what you wanted
Kama nkupigie simu nkusikie tu itanitosha
Hata ukinitukana moyo wangu utaupumzisha (baby come back)
Kama wakati urudi nyuma uniombe msamaha tena
Ama usingenikosea tuishi kama zama
Ukirudi sikuachi uende tena
Hata ukinikosea ukafanya ka' uliyoyafanya tena
Nani atafanya nisikuwaze? Hakuna binti wa aina yako
Nsasamehe ulikosea tu rudi kwa nafasi yako (rudi maa!)
Sileti tena kisu kwenye mpambano wa bunduki
Shell silingi tena taka sitaki sasa basi

[Bridge - Dojo&Domo]
Nikikaa chini waza mengi juu yako
Na some times, na-miss sana hot kisses zako
Natamani niguse tena mwili wako
Penzi lako, natamaniiiihh kama zamaniiii!!

[Hook+Outro - Dojo,Domo&FA]
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani (kama kama kama kama zamani)
Natamani iwe Eeh!
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani (kama kama kama kama zamani)
Natamani iwe Eeh!

One more time..

Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani
Natamani iwe Eeh! (Lete kwaya sasa!)
Oh oh oh! natamani iwe, natamani iwe kama zamani
Natamani iwe...Eeh!

No comments:

Post a Comment