walalahoi by Izzo business


Intro:
Walala hoi…
Walala hoi…
Walala hoi

Chorus:
Walala hoi sisi ndio Walala hoi (Walala hoi) x 4
moja haikai mbili haikai mbaya wako ni jirani babu (Walala hoi) x 4

Verse 1:
Tunaunga unga maisha yetu ni safari bado tunataabika (Walala hoi)
tunakomaa maisha ni safari imani ipo bado sisi mbali tutafika (Walala hoi)
tumazaliwa kwenye njaa njaa imetulea sisi home mali hatujakuta (Walala hoi)
mama Yanga baba Simba upinzani babu ndani yani kila dakika (Walala hoi)
kupinda ni sheria usishangae huku kwetu mbona imeshazoeleka (Walala hoi)
hatujasoma dili chafu leta pesa babu hata iwe dili ya kuteka (Walala hoi)
 tunaonekana hatuna maana tunatengwa kona zote twa dharaulika
majina yote sisi Vidampa wapumbavu wezi majambazi yote wametupachika 
Rhumba kali wewe utadata
soma pata ondoa shaka
faster umenipata chafu tatu maisha karata
maisha bondi kukosa na kupata
jela nyummbani hakuna kuogopa sheli tunamoka
sisi machizi kama kaboka
uchungu wa meno na kucha kamuulize Ulimbok

Chorus:
Walala hoi sisi ndio Walala hoi (Walala hoi) x 4
moja haikai mbili haikai mbaya wako ni jirani babu (Walala hoi) x 4

Verse 2:
Roba za mbao mtaani ni nani kaleta? (Walala hoi)
kulogana logana tu bila sababu mtaani? (Walala hoi) 
majungu fitina unafiki umbea na chuki? (Walala hoi) 
kazi ngumu tunapigika lakini ujira ni mdogo babu (Walala hoi)
toa kazi tumalize hatulazi kitu hapa sisi mwendo ni wa CHAP-CHAP
kwenye Bar hatukai zetu vilabuni yes sisi mwendo ni MATAPU-TAPU 
bila sababu tunakudiss tukijua umetuzidi sisi wala hatukukwepeshi
chuki roho mbaya jadi yetu Mungu hapendi lakini sisi tumerithi
kila time tupo simple watu wa Mingle mawazo yetu kwenye Bingo dr.Kingo ngoma zetu ni Segere na Msondo
sisi ndio wachezeshaji tuite Redondo
Rest in Peace James mtoto wa Dandu 
hii game bado kwako japo upo kando 
big brother the Chase muulize Nando
kama Zay-B vile watu wapo gado

Chorus:
Walala hoi sisi ndio Walala hoi (Walala hoi) x 4
moja haikai mbili haikai mbaya wako ni jirani babu (Walala hoi) x4

Outro:
Walala hoi…
Walala hoi…
Walala hoi…
Walala hoi x 3…
hoi hoi hoi Walala …
hoi hoi hoi Walala…
hoi hoi hoi Walala.

No comments:

Post a Comment